• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

Wananchi wafurahia upanuzi wa kituo cha Afya Kilimarondo

Imetumwa : July 20th, 2018

Wananchi wafurahia upanuzi wa kituo cha Afya Kilimarondo

Wananchi wa Tarafa ya Kilimarondo wameishukuru na kuipongeza Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe magufuli kwa kuleta fedha kwa ajili ya upanuzi wa kituo cha afya Kilimarondo

Waliyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mheshimiwa Godfreya Zambi alipofanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa majengo mapya katika kituo hicho cha Afya jana , kilichopo takribani Kilomita 90 kutoka Nachingwea mjini.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais John Magufuli kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo haya, kwani isingelikuwa yeye tusingepata majengo haya yatakapokamilika yatatusaidia sana” Alisema Ephrostina Jastin

Naye ndugu Salum Pilikano amesema kwa mda mrefu Kituo cha afya Kilimarondo kimekuwa hakina huduma za upasuaji lakini wanaamini mara baada ya kukamilika kwa kituo hicho huduma hizo zitakuwa zikipatikana katika maeneo hayo na hivyo kupunguza gharama za kupata huduma za afya.

Wananchi hao wamedai kuwa baada ya kukamilika kwa kituo hicho vifo vya mama na mtoto vitapungua kwani kutokana na umbali wakina mama wamekuwa wakijifungulia njiani na nyakati zingine wamekuwa wakifariki kutokana umbali kutoka Kilimarondo hadi ilipo hospitali ya Wilaya.

Aidha Mkuu wa Mkoa ameipongeza Halmashauri kwa usimamizi mzuri hadi mradi ulipofikia, na kutaka usimamizi uendelee ili kukamilisha mradi huo kwani umaliziaji usipokuwa mzuri kazi ya ujenzi wa majengo hayo utakuwa hauna maana.

“Katika hatua hii huwezi kuona dosari, tuongeze usimamizi kwenye ‘finishing’ kwani mafundi wengi wanapata shida sana kwenye hatua hizi” Alisema Mheshimiwa Zambi.

Kituo cha Afya Kilimarondo ni miongoni mwa vituo vituo vya afya nchini vilivyopewa Shilingi milioni 400 kwa ajili ya kujenga majengo mapya ya kutolea huduma, ambapo katika kituo hicho majengo ya jengo la maabara, jengo kujifungulia mama wajawazito, jengo la upasuaji na jengo la kufifadhia maiti yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANAFUNZI WA NACHINGWEA HIGH NA RUGWA BOYS WAAGWA KWA HAFLA FUPI, WAJIANDAA KWA MITIHANI YA TAIFA

    April 26, 2025
  • SDA NA LIIKE WATOA MAFUNZO YA HUDUMA YA KWANZA KWA MANGALIBA NA WALOMBO KWA AJILI YA KUIMARISHA UTAMADUNI SALAMA

    April 28, 2025
  • DED NACHINGWEA : AAGIZA MIRADI KUKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA KUZINGATIA VIWANGO

    April 09, 2025
  • RC LINDI : MIRADI YOTE ITAKAYOPITIWA NA MWENGE IZINGATIE MATUMIZI BORA YA FEDHA

    April 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.