• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

WAANDISHI WASAIDIZI VITUONI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAAPISHWA NACHINGWEA

Imetumwa : May 14th, 2025


Leo tarehe 14 Mei 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea imeendesha mafunzo ya siku moja kwa Waendesha Vifaa vya BVR (Biometric Voter Registration) na Waandishi Wasaidizi wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa ajili ya uboreshaji awamu ya pili ya uandikishaji.


Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa shule ya Nachingwea Day na yamefunguliwa rasmi na Afisa Mwandikishaji Wilaya ya Nachingwea, Mhandisi Chionda Kawawa. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Kawawa amewataka washiriki wote kuzingatia kiapo walichoapa kwa dhamira ya kweli, kwa kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi, uadilifu na uzalendo kwa taifa.


“Tumepata dhamana hii kubwa ya kuhakikisha kila Mtanzania mwenye sifa anapata nafasi ya kuandikishwa. Hili ni jukumu la kitaifa, hivyo ni lazima tulitekeleze kwa uaminifu na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote za Tume ya Taifa ya Uchaguzi,” alisema Mhandisi Kawawa.


Afisa Mwandikishaji pia amesisitiza umuhimu wa teknolojia ya BVR katika kuhakikisha usahihi na ufanisi wa mchakato wa uandikishaji, akieleza kuwa matumizi sahihi ya vifaa hivyo ni msingi wa kuwa na daftari la kisasa, sahihi na linaloaminika.


Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo washiriki katika kutumia vifaa vya BVR kwa usahihi, kuelewa taratibu za uandikishaji pamoja na namna ya kushughulikia changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.


Aidha, Halmashauri ya Nachingwea inatoa wito kwa wananchi wote wenye sifa za kuandikishwa, kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura ambalo litaanza rasmi tarehe 16 Mei hadi 22 Mei 2025, wananchi wanakumbushwa kufika katika vituo walivyojiandikisha  awali kukagua taarifa zilizobandikwa katika vituo hivyo. Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora.


Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MWENGE WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 2.2 CHANGAMOTO ZA MAJI,AFYA ZA MALIZWA WANANCHI WAFURAHIA NISHATI SAFI

    May 29, 2025
  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WATAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU KWA AWAMU YA PILI

    May 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA BARABARA KIWANGO CHA LAMI NACHINGWEA

    May 29, 2025
  • RUNALI YAANZA MAANDALIZI YA MSIMU WA UFUTA NA MBAAZI KWA MSINGI WA UBORA NA UWAJIBIKAJI

    May 28, 2025
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.