Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Dokta. Steven Kiruswa kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kilele cha Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Lindi, Juni 14, 2025 Wilayani Ruangwa, amesema Wizara ya Madini inafahamu umuhimu wa ushiriki wa wachimbaji wadogo katika sekta ya Madini hivyo inaendelea kutoa elimu, tekinolojia ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini.
Dkt Kiruswa amesema serikali imeandaa mazingira bora kwa wachimbaji wadogo kwa kuanzisha leseni ndogo kwa ajili ya wachimbaji wadogo, amesisitiza kwamba sekta ya madini inasimamiwa vizuri na masoko yameongezeka kutoka 1 hadi kufikia 43 kwa sasa.
Hivyo ili kuongeza thamani serikali inataka madini yetu kuchimbwa na kuchakatwa hapahapa nchini na sio kupelekwa nje ya nchi kama ambavyo inafanyika sasa kwa baadhi ya madini, hvyo serikali ipo katika mchakato wa kulifanikisha hilo.
Pia, ametolea ufafanuzi swala la leseni kwa wachimbaji wa mgodi wa Nditi, amesema serikali imelipokea swala hilo la kupatiwa leseni na ipo njiani kulifanyia utatuzi hivyo wana Nditi wanaombwa kuwa na subira kwani hivi karibuni jambo lao la muda mrefu litatimia.
Aidha, Kwa niaba ya Waziri Mkuu amesisitiza wananchi wote kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ili kutimiza malengo na maslahi ya nchi ambayo yalianza kutekelezwa tangu awamu ya sita ilipoingia madarakani.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.