Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Mhandisi Chionda M. Kawawa alipokua katika hafla fupi ya kuwaaga Madiwani iliyofanyika Juni 20, 2025 katika ukumbi wa Mondolane Mesi Wilayani Nachingwea.
Mhandisi Chionda ametoa pongezi kwao kwa ushirikiano waliouonesha katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2020 hadi 2025, katika wakati wao ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutokea bilion 2.2 hadi kufikia bilion 5.6 ambazo ni sawa na 249%, pia mavuno ya zao la korosho yameongezeka kutoka milioni 15 hadi kufikia kilo milioni 23.
Aidha, Mwenyekiti wa Halmashauri aliyemaliza muda wake mheshimiwa Adinan Mpyagila ametoa pongezi na shukrani kwa ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kwa kazi nzuri wanazozifanya kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Nachingwea na kushirikiana vizuri na Madiwani.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.