• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

KAMATI YA SIASA MKOA (LINDI) YAFURAHISHWA NA MIRADI YA BILION 3.6 NACHINGWEA

Imetumwa : February 11th, 2026

Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Lindi imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo na hatua mahususi zinazochukuliwa kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

Pongezi hizo zimetolewa na wajumbe wa kamati hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani Nachingwea,  ziara hiyo imeongozwa na Katibu wa Siasa wa Mkoa wa Lindi, Ndugu Barnabasi Essau.

Katika ziara hiyo, kamati ilikagua miradi mitatu mikubwa ikiwemo ujenzi wa Jengo Jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, ujenzi wa Barabara ya KKKT kuelekea Hospitali ya Wilaya, pamoja na ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi na Awali katika eneo la Shule ya Sekondari Stesheni.

Miradi hiyo yenye thamani ya shilingi bilioni 3.6 ipo katika hatua za ukamilishaji, jengo jipya la utawala limefikia asilimia 80 ya utekelezaji na linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni tatu, Barabara ya KKKT yenye urefu wa kilomita 0.5 imegharimu shilingi milioni 356, huku ujenzi wa shule ya msingi na awali ukiwa katika hatua za mwisho kwa gharama ya shilingi milioni 314.


Akizungumza mbele ya wananchi wa eneo la Stesheni, Ndugu Essau alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mheshimiwa Mohamed Hassan Moyo pamoja na timu ya wataalamu wa halmashauri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Mhandisi Chionda M. Kawawa kwa kutekeleza Ilani ya Chama kwa ufanisi.


“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, niwashukuru na kuwapongeza wewe pamoja na timu ya wataalamu kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Tumetembelea miradi mitatu ambayo ipo katika hatua za mwisho za ukamilishaji, hivyo nitoe wito ikamilike kulingana na ratiba iliyopangwa,” alisema Essau.


Kwa upande wao, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa walieleza kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na uongozi wa halmashauri, wakisisitiza umuhimu wa kuendelea kusimamia miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati na kuleta tija kwa wananchi.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. DIWANI ATOA MOTISHA KUENDELEZA UFAULU, ASISITIZA LISHE SHULENI

    February 11, 2026
  • KAMATI YA SIASA MKOA (LINDI) YAFURAHISHWA NA MIRADI YA BILION 3.6 NACHINGWEA

    February 11, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI LARIDHIA MPANGO MPYA BAJETI 2026/2026, DED CHIONDA ASISITIZA USHIRIKIANO

    February 12, 2026
  • MHE. DIWANI KATA YA STESHENI ATOA MOTISHA KWA WAALIMU SEKONDARI YA STESHENI

    February 05, 2026
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.