Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea limefanya mkutano wake kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kwa lengo la kupitia na kujadili kwa kina ajenda mbalimbali zilizopangwa.

Mkutano huo umeongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Mhandisi Chionda A. Kawawa, na umefanyika leo tarehe 11 Februari, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri. Mkutano huo umewakutanisha wajumbe kutoka idara mbalimbali za Halmashauri, waliopata fursa ya kuchangia hoja na kutoa maoni yao.

Katika mjadala huo, wajumbe walieleza kuridhishwa na mapendekezo ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027, wakisisitiza umuhimu wa kuendelea kupanga na kutekeleza mipango kwa kuzingatia vipaumbele kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi.
Mhandisi Kawawa amewahimiza watumishi kuendeleza ushirikiano, mshikamano na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Amesisitiza kuwa umoja, nidhamu na uwazi ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya taasisi na kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi.
Aidha, Dokta Samwel Magero, ambae ni Katibu TUGHE Mkoa wa Lindi, amepongeza namna wajumbe wa kikao hicho walivojitokeza kwa wingi na kuonesha ushirikiano katika kuchangia, pia amewsisitiza wajumbe kuhakikisha yale yote yaliyojadiliwa wanakwenda kuyafanyia kazi hususani katika utekelezaji wa mipango mbalimbali kulingana na bajeti iliyojadiliwa.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.