Mkuu wa Wilaya yaNachingwea Mheshimiwa Mohamed Hassan Moyo amewataka Watendaji wa Kata kuhamasisha upatikanaji wa chakula mashuleni na kuifanya kua miongoni mwa ajenda ya kudumu katika mikutano ya jamii na vikao vya uongozi ili kuhakikisha kila shule inatoa chakula.
Hayo yamezungumzwa leo Juni 17, 2025 na Mkuu wa wilaya huyo katika kikao cha tathmini ya lishe cha robo ya tatu 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Halmashauri ya wilaya Nachingwea.
Mheshimiwa Moyo amesema kuhamasisha ukusanyaji chakula cha mwaka mzima mashuleni itasaidia kujihakikishia uwepo wa chakula lakini pia kuondoa changamoto ya kukosa chakula ifikapo katikati ya mihula ya masomo.
Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nachingwea Mhandisi Chionda Kawawa amewapongeza kitengo cha lishe kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhamasisha na kufuatilia suala zima la lishe.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.