• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

DC MOYO AWATAHADHARISHA WAKULIMA UWEPO WA MVUA CHACHE, AWASIHI WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Imetumwa : February 19th, 2026

Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Mheshimiwa Mohamed Hassan Moyo, ametoa tahadhari kuhusu mwenendo wa mvua kutokuwa mzuri kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Amesema kuwa kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), maeneo ya Wilaya ya Nachingwea yanatarajiwa kupata mvua za wastani au chini ya wastani.

Ameyasema hayo leo, Februari 19, 2026, alipokuwa katika Mkutano wa Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC). Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kiwango cha mvua kinatarajiwa kuwa kati ya milimita 940 hadi 1000 kwa msimu, huku kukiwa na uwezekano wa baadhi ya maeneo kupata mvua chini ya milimita 940, hali itakayokuwa chini ya wastani.

Taarifa iliyotolewa na TMA inaonesha kuwa hali hiyo inaweza kuathiri uzalishaji wa mazao, hasa mazao ya biashara kama ufuta, mbaazi na korosho katika Wilaya ya Nachingwea. Kutokana na hali hiyo, Mheshimiwa Moyo amewataka viongozi wa ngazi za kata kuhakikisha wanashirikiana na wataalamu wa kilimo kutoa elimu kwa wakulima ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.


Kwa upande mwingine, Mheshimiwa Moyo ameendelea kukumbusha na kusisitiza umuhimu wa elimu kwa watoto. Amesema kuwa moja ya haki muhimu ya mtoto ni kupata elimu, na kusisitiza kwa wazazi kuwa ni wajibu wao kuhakikisha watoto wanapata elimu. Aidha, amewataka viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa na machifu kuhakikisha watoto wote wanaostahili kwenda shule wanakwenda. Amesisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na miundombinu mbalimbali ili kuboresha mazingira ya kujifunzia. Aliongeza kuwa elimu ni msingi wa ustawi wa mtoto na taifa kwa ujumla.


Sambamba na hilo, Mheshimiwa Moyo amekumbusha umuhimu wa maadili katika malezi ya watoto na kuhimiza malezi yenye usawa bila upendeleo wa kijinsia, akisisitiza kuwa watoto wote wana haki sawa na ni mhimili wa familia na taifa.


Aidha, amesihi wakazi wa Wilaya ya Nachingwea kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo wilayani humo, ikiwemo kilimo, mifugo na hasa sekta ya madini, ili kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja, wilaya na taifa kwa ujumla. Pia amewataka wakulima wenye mashamba katika maeneo yenye madini kutouza ardhi yao kiholela.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC MOYO AWATAHADHARISHA WAKULIMA UWEPO WA MVUA CHACHE, AWASIHI WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

    February 19, 2026
  • MHE. DIWANI ATOA MOTISHA KUENDELEZA UFAULU, ASISITIZA LISHE SHULENI

    February 11, 2026
  • KAMATI YA SIASA MKOA (LINDI) YAFURAHISHWA NA MIRADI YA BILION 3.6 NACHINGWEA

    February 11, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI LARIDHIA MPANGO MPYA BAJETI 2026/2026, DED CHIONDA ASISITIZA USHIRIKIANO

    February 12, 2026
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.