• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

FURUSA ZA BIASHARA WILAYANI NACHINGWEA

FURUSA ZA BIASHARA HALMASHAURI YA WILAYA  YANACHINGWEA

 

UTANGULIZI

 

Wilaya ya Nachingwea ipo umbali wa km 140 kutoka makao makuu ya mkoa wa Lindi  , ipo kati  ya  nyuzi  10 - 11  Latitude  kusini   mwa    ikweta  , nyuzi 38 - 39 longitudo mashariki mwa griniwich.Nachingwea inapakana na Wilaya ya Ruangwa kwa upande wa kaskazini - mashariki ,Wilaya ya Masasi upande wa Kusini - mashariki ,Wilaya ya Tunduru upande wa kusini -magharibi na Wilaya ya Liwale upande wa Kaskazini - magharibi.Wilaya zingine zilizopo katika Mkoa wa Lindi ni Wilaya ya Kilwa, Manispaa ya Lindi na Wilaya ya Lindi Vijini.

WAKAZI 

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.Wilaya ya Nachingwea ilikuwa   na Jumla ya wakazi wapatao 178,464 ambapo 86,382 wavulana   na      92,082 wanawake

UCHUMI

Pato la jumla la wakazi wa Nachingwea (GNP) kwa mwaka 2015/2016, lilikuwa Tshs 65,139,360,000/= (Bilioni sitini na tano milioni mia moja thelethini na tisa mia tatu sitini elfu tu.) Wastani wa pato la wakazi wa Nachingwea (Per Capital income) kwa mwaka 2015/2016 lilikuwa Sh 365,000/= kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.

Nachingwea ina ardhi yenye rutuba, hivyo kuwezesha uzalishaji wa mazao mengi ya chakula na biashara. Fursa hii itasaidia Wilaya yetu kutimiza dhana ya ‘KAZI IENDELEE’ na hatimae kufikia malengo ya uchumi wa kati. Katika kutekeleza majukumu ya kuinua uchumi, kupitia

 



  • FURSA ZINAZOPATIKANA SEKTA YA BIASHARA

Kufungua biashara Mjini na Vijijini:

Biashara za maduka ya rejareja.

Biashara za maduka ya nusu jumla.

Biashara za maduka ya jumla.

Biashara za vileo.

Biashara za nyumba za wageni.

Biashara za kumbi za mikutano.

Biashara za maduka ya pembejeo za kilimo.

Biashara za maduka ya dawa muhimu.

Biashara za maghala ya kuhifadhia mazao.

Biashara ya kufungua Kiwanda.

Biashara ya kufungua Shule binafsi.

Biashara ya kufungua Vyuo binafsi.

Biashara za vituo vya kuuza mafuta.

Biashara za kuuza nafaka.

Biashara za maduka ya vifaa vya ujenzi.

Biashara ya Vituo Vya afya na hospitali binafsi.

Biashara ya Super Market.

Biashara za vifaa vya michezo.

Bank.

Biashara ya Uwakala wa Mabenki.

Biashara ya fedha kupitia uwakala wa mitandao ya simu.

Kuuza mitungi ya gesi na majiko ya gesi.

Na biashara nyinginezo.

 

 



3.0 HALI YA UTOAJI WA LESENI ZA BIASHA NACHINGWEA

S/N

MWAKA

IDADI YA LESENI

PATO LINALOTOKANA NA  ADA  ZA LESENI ZA BIASHARA

1.
2015/2016 (JULAI /JUNI)
732
32,783,400.00
2.
2016/2017 (JULAI / JUNI)
755
40,185,000.00
3.
2017/2018 (JULAI / JUNI)
696
33,520,500.00
4.
2018 /2019 (JULAI/JUNI)
791
40,474,000.00
5.
2019/2020 (JULAI/JUNI)
446
27,761,600.00
6.
2020/2021 (JULAI/JUNI)
350
29,566,000.00
7.
2021/2022(JULAI/SEPTEMBA……..)
181
16,864,000.00

 

 

CHATI KUONESHA HALI YA MAKUSANYO YATOKANAYO NA ADA ZA LESENI ZA BIASHARA KATIKA WILAYA YA NACHINGWEA

 

 

 

CHANGAMOTO

  • Kuhama kimakazi kwa wafanyabiashara kutoka wilaya ya Nachingwea na  kwenda nje ya Nachingwea. 
  • Kutokea kwa vifo kwa mfanyabiashara.
  • Kuacha biashara.
  • Biashara ya msimu zinazosajiliwa wakati wa mavuno ya kilimo cha ufuta na korosho - zizokuwa na muendelezo baada ya msimu kwisha na kuacha madeni (defaulters) kwenye mfumo wa kielektroniki wa kukusanyia mapato. Mf; Biashara.
  • Kufilisika.
  • Kubadilika kwa taratibu mbalimbali za biashara.
  • TAARIFA YA UGAWAJI WA VITAMBULISHO VYA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WATOA HUDUMA WADOGO (WAMACHINGA).
  •  
  •  
  • S/NA
  • MWAKA
  • VITAMBULISHO VILIVYOPOKELEWA
  • VITAMBULISHO VILIVYOUZWA
  • KIASI KILICHOKUSANYWA
  • 3
  • 2019/2020
  • 15,000
  • 9500
  • 190000000.00
  • 4
  • 2020/2021
  • 9500
  • 3556
  • 71120000.00
  • 5
  • 2021/2022
  • 6000
  • 636
  • 12,720,000.00

 

  •  
  • CHANGAMOTO
  •  
  • Wajasiliamali wengi kutegemea kupata huduma ya vitambulisho vya mjasiriamali ofisi ya biashara na ofisi za watendaji kata tu hali ya kuwa mfumo kielektroniki wa vitambulisho vya mjasiriamali unapatikana kwenye simu za mkononi na wanaweza kujihudumia wenyewe hadi kufikia hatua ya kupata namba ya malipo na kuweza kulipia kitambulisho cha mjasiliamali.
  • Wajasiriamali wengi shughuli zao za ujasiriamali hazina muendelezo, leo anakuwa na shughuli ya kijasiriamali ya kuhitaji kuwa na kitambulisho na baada ya muda mfupi shughuli hiyo inakosa muendelezo na kupoteza sifa ya kumiliki kitambulisho cha Mjasiriamali.
  • Kuhama makazi kwa Mjasiriamali kutoka Wilaya ya Nachingwea na kuhamia wilaya nyingine.
  • Kutokea kwa cha Kifo kwa Mjasiriamali.

MASOKO

 

Nachingwea ina jumla ya masoko manne yanayomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea.Wanachi upata mahitaji yao mbalimbali kutoka katika masoko hayo. Mji wa Nachingwea Wakazi wake Wanaongezeke na hivyo kutakuwa na ongezeko la Masoko kadri idara ya Maliasili na ardhi inavyopima viwanja vya makazi ya Watu. Masoko yaliyopo kwa sasa ni:

1. SOKO KUU NACHINGWEA

2. SOKO LA VODA

3. SOKAO LA TUNDURU YA LEO

4. SOKO LA MATUNDA.

MABENKI

 

Nachingwea ina jumla ya benki tatu zinazotumiwa na wakazi wa Nachingwea.Kukua kwa teknolojia kumesaidia shughuli za kibenki kujitanua na kutoa furusa za wananchi kujiajiri kwa kuwa na Mawakala wa benki katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Nachingwea na kuwarahisishia wananchi kufanya malipo ya ankara mbalimbali, kutuma na kupokea fedha toka ndani na nje ya Nachingwea. Benki hizi ni:

1. NMB

2. CRDB

3. TCB

HUDUMA ZA FEDHA (MICROCREDIT)

 

Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea ina watoa huduma za kifedha (microcredit) wanaotambuliwa na serikali kwa leseni walizonazo toka Benki kuu ya Tanzania (BoT) na Brela wapatao kumi na moja ambao ofisi zao zipo Nachingwea Mjini katika mitaa tofautitofauti. Watoa huduma hawa utoa mikopo yao ya fedha kwa watumishi na watu mbalimbali na hivyo husaidia sekta ya biashara kwa wanufaika wa mikopo inayotolewa. Watoa huduma waliopo kwa sasa ni:

1.ABC BANK

2. MABOTO ENTERPRISES

3. SUMUNI CREDIT

4. CHOGO CREDIT

5. MAGERE CREDIT

6. WILIUM CREDIT

7.WICOM FINANCE LTD

8. TATA CREDIT

9. PLATNUM CREDIT

10. SILVER MICROFINANCE

11. FAIDIKA

MITANDAO YA MAWASILIANO

 

Halmashauri ya Nachingwea ina jumla ya mitandao ya mawasiliano sita na kufanya mawasiliano kupatikana kwa simu za kiganjani kwa wakazi wengi wanaoishi maeneo mbalimbali ya Nachingwea kuwasiliana kwa urahisi wakati wote. Aidha kupitia mitandao ya simu wanachi utumia fursa hiyo kujiajiri kwa kuwa Mawakala na kuwarahisishia wanachi kupata huduma ya kutuma na kupokea pesa kwa ndugu na marafiki kwa njia ya simu katika maeneo mbalimbali ya nachingwea nan je ya Nachingwea. Mitandao ya mawasiliano iliyopo kwa sasa ni:

1. TIGO

2. VODA

3. AIRTEL

4. HALOEL

5. TTCL

6. ZANTEL

 

 

4.0 HALI YA UWEKEZAJI

 

HALI YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MADINI

 

  • Aina za Madini zinazopatikana katika Wilaya ya Nachingwea
  • Fursa zilizopo
  • Kinachofanyika kwa sasa
  • Changamoto zilizopo na Mikakati

Wilaya ya Nachingwea ni Wilaya iliyobarikiwa kuwa na madini ya aina nyingi. Kiwango cha uwekezaji kwa maana ya umiliki wa leseni za utafiti na uchimbaji/uchakataji pamoja na leseni za biashara ya madini ni cha chini. Miradi mingi ya utafiti na uchimbaji wa madini haiendelezwi ili kufikia hatua ya uchimbaji na hata wawekezaji wengi wenye leseni ndogo za uchimbaji hawazifanyii kazi (undeveloped).

Mada hii inalenga kuainisha aina za madini na maeneo yaliyopo katika Wilaya ya Nachingwea, fursa mbali mbali za uwekezaji zilizopo katika sekta ya madini katika Wilaya ya Nachingwea, pia taarifa hii itapambanua shughuli mbalimbali zinazofanyika katika sekta ya madini katika Wilaya hii. Na mwisho itabainisha changamoto mbalimbali zilizopo katika sekta ya madini katika Wilaya ya Nachingwea na kutoa maoni ya namna ya kutatua changamoto hizo.

 

 

AINA ZA MADINI ZINAZOPATIKANA KATIKA WILAYA YA NACHINGWEA

 

Madini yaliyopo katika Wilaya ya Nachingwea ni madini ya metali, vito, viwandani na madini ya ujenzi. Jedwali namba 1 linaonesha maeneo mbalimbali madini hayo yanapopatikana na hali halisi ya kinachoendelea kwa sasa katika maeneo hayo.

 

 

 

Jedwali na. 1: Aina za Madini yaliyopo katika Wilaya ya Nachingwea 

AINA YA MADINI
ENEO/KIJIJI
HALI YA UCHIMBAJI
Dhahabu (Gold)
Mto Mbwemkuru,
Ngapa, Ikungu, Maguja, marambo
Uchimbaji unafanyika
Saphire
Ulanga, Cobalt, Nikeli, Magnesite
Nachingwea
Uchimbaji haufanyiki
Nikeli, Shaba, Cobalt
Lionja
Uchimbaji haufanyiki
Ulanga
Kitati
Uchimbaji haufanyiki
Kinywe (Graphite), Marble
Mkotokuyana
Uchimbaji haufanyiki
Kinywe (Graphite)
Chilunga
Uchimbaji haufanyiki
Ulanga
Mianganda
Uchimbaji haufanyiki
Ulanga
Mbuti
Uchimbaji haufanyiki
Kinywe (Graphite)
Nammanga
Uchimbaji haufanyiki
Nikeli, Shaba, Cobalt
Ntaka
Uchimbaji haufanyiki
Ulanga
Majiane
Uchimbaji haufanyiki
Kinywe (Graphite)
Chilunga
Uchimbaji haufanyiki
Mchanga, Kifusi, mawe
Nachingwea
Uchimbaji unafanyika

FURSA ZILIZOPO KATIKA SEKTA YA MADINI 

  1. Fursa za moja kwa moja

Umiliki wa leseni za Kuchimba (SML, ML, PML)

Umiliki wa leseni za biashara ya Madini (Brokers na Dealers)

Umiliki wa mitambo ya kuchenjulia madini (cyanidation plant)

Umiliki wa mitambo ya uchimbaji kwa ajili ya kukodisha

Ufundi mitambo; mfano winchi, magari na mitambo ya aina nyingine

Chakula: Migahawa, hoteli na Mama Lishe

Ardhi/Nyumba: Ununuzi au ukodishaji wa maeneo kwa ajili ya uchimbaji, makazi au shughuli za kiufundi

Usafiri: Uwepo wa shughuli za usafirishaji

 

 

 

 

 

Kinachoendelea kwa sasa 

AINA YA LESENI 
IDADI YA LESENI 
HALI YA SASA (STATUS) 
MAELEZO 
RL
1
MAANDALIZI YA KUJENGA MGODI
Leseni hii ni mali ya Serikali anatafutwa mzabuni wa kuwekeza katika eneo hili.
ML
03
UCHIMBAJI/ MAANDALIZI YA KUJENGA  MIGODI
Kumekuwa na hali ya kusua sua katika uendelezaji wa miradi hii.
PL
21
UTAFITI
Kumekuwa na hali ya kusua sua katika uendelezaji wa miradi hii.
PML
199
UCHIMBAJI/ LIOLALA (DORMANT)
Ufutaji wa leseni zisizoendelezwa unaendelea kwa mujibu wa sheria.
Dealers
1

-

-

Brokers
4

-

-

MASOKO YA MADINI 
VITUO VYA UNUNUZI (BUYING CENTRES) 
MAELEZO 
SOKO LA MADINI RUANGWA
NAMUNGO- DHAHABU/ VITO


KIEGEI-DHAHABU/ VITO

Na. 
Changamoto 
Hatua iliyochukuliwa 
Mkakati 
1.
Umbali wa eneo la kununulia milipuko (baruti, n.k.) ambao huongeza gharama za kusafirisha mara kwa mara hasa kwa wachimbaji wadogo.
Umefanyika uwekezaji katika eneo la karibu (Kilwa) na kampuni ya Nitro Explosives.
Kumwezesha mwekezaji huyu kuanza uzalishaji mapema iwezekanavyo
2.
Barabara kutoka maeneo ya uchimbaji sio nzuri na hazipitiki muda wote. Hali hii husababisha wachimbaji wengi kusimamisha shughuli za uzalishaji kipindi cha mvua.
Uandaaji wa mpango wa ujengaji yadi katika maeneo ya uchimbaji ambapo barabara kutoka machimboni hadi kwenye yadi na kutoka kwenye yadi hadi barabara kuu zitaboreshwa ziweze kupitika muda wote.
Kuwashirikisha wadau wote  (Wachimbaji na wenye viwanda) katika kuchangia ili kupata fedha za kufanikisha mpango huu
3.
Ufinyu wa mitaji (kusababisha gharama za uzalishaji kuwa kubwa, hasa kwa PMLs (Prod.Cost/tonne)-kushindwa kutengeneza miundo mbinu, kufanya kazi miezi michache kwa mwaka kusimamisha uzalishaji wakati wa mvua), kukodi mitambo kwa zamu.
Utaratibu wa kutoa elimu juu ya fursa mbalimbali za kupata mikopo katika taasisi za fedha umekuwa ukifanyika kwa kushirikiana na taasisi za kifedha.

4.
Kutokuwa na tabia ya kuweka kumbukumbu za uzalishaji wa na gharama zake hivyo kushindwa kupata mikopo lakini hata wanapopata mikopo hushindwa kulipa kutokana na kushindwa kutambua faida ni kiasi gani hali ambayo husababisha kufilisika.
 Wachimbaji wameendelea kupatiwa elimu ya namna ya kuendesha biashara zao.

5.
Ukosefu wa viwanda vya kupandisha thamani (Refining) kusababisha madini mengine kutochimbwa kabisa Mn, Cu, Co etc.
Uhamasishaji uliofanywa na Serikali umeanza kuonesha mafanikio kwa viwanda vidogo vya kusafisha shaba kujengwa nchini na hivyo uchimbaji wa shaba ghafi kuwa na soko la uhakika.
Hivi karibuni Serikali imefanya marekebisho katika muongozo uliokuwa unatumika ambao una taratibu za uongezaji thamani “Mining (Value Addition) Regulations, 2020 ambapo imelegeza masharti ili kuwawezesha wachimbaji wadogo wasikwame.
Kuendelea kuhamasisha iliuwekezaji zaidi kwa madini mengine ufanyike

MAZAO YA BIASHARA

HALI YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA KILIMO ZAO LA KOROSHO

 

Hali ya uzalishaji wa zao la korosho

 

S/Na
MWAKA
TANI
1
2017/2018
21
2
2018/2019
16
3
2019/2020
16
4
2020/2021
22
5
2021/2022
23

 

MIKAKATI YA KUENDELEZA UWEKEZAJI ZAO LA KOROSHO

 

Wilaya inafanya juhudi nyingi kuhakikisha uwekezaji mkubwa unafanyika. Juhidi hizo ni pamoja na kuanzisha mradi wa mbegu bora za zao la korosho kijiji cha Likwela kata ya Mkoka (mradi huu ushaanza msimu uliopita wa kilimo 2020/2021). Juhudi nyingine ni pamoja na kuendeleza viwanda na kuongeza ufanisi katika viwanda vya korosho.

4.2 UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA KILIMO ZAO LA UFUTA

 

Hali ya uzalishaji wa zao la ufuta

 

S/Na
MWAKA
TANI
1
2017/2018
2,383
2
2018/2019
4,070
3
2019/2020
8,500
4
2020/2021
10,300
5
2021/2022
7,493

MIKAKATI YA KUENDELEZA UWEKEZAJI ZAO LA UFUTA

 

Wilaya inafanya juhudi nyingi kuhakikisha uwekezaji mkubwa unafanyika. Juhidi hizo ni pamoja na kuanzisha mradi wa mbegu bora za zao la ufuta kijiji cha Likwela kata ya Mkoka (mradi huu utaanza msimu ujao wa kilimo). Juhudi nyingine ni pamoja na kuendeleza viwanda na kuongeza ufanisi katika viwanda vya korosho.

4.2 Uwekezaji katika sekta ujasiliamali vikundi vya ujasiriamali 

Jumla ya vikundi 300 vya ujasiriamali vimesajiliwa. Vikundi hivi vinajishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi hasa Mama lishe, Bodaboda, VICOBA, kushona mavazi, ufugaji, kilimo, ufundi seremala, kuchomea chuma, usindikaji, kubangua korosho, uhunzi na uchongaji.

JEDWALI LA VIKUNDI VYA UJASILIA MALI

 

S/NA
IDADI YA VIKUNDI
SHUGHULI 
1
15
Kilimo cha mbogamboga
2
40
Ufugaji
3
10
Korosho
4
2
Ufuta
5
19
Labourbase
6.
1
Vinyago
8.
1
Uhunzi
9.
212
Vikoba,Bodaboda,Mama Lishe,Kushona n.k
Jumla
300
 

 

4.3 Uwekezaji katika sekta ya viwanda 

Jumla ya viwanda vidogo vidogo 134 vimesajiliwa hapa Wilayani.Shuguli kubwa ya viwanda hivi ni kutengeneza samani, ushonaji, usindikaji, Ubanguaji korosho na kusaga nafa.

JEDWALI KUONESHA VIWANDA 

S/NA
KIWANDA
SHUGHULI
ENEO
1
1
Ubanguaji wa korosho
Nangowe
2
5
Kutengeneza samani
Eneo la viwanda, Mtua,T/Leo, Ugogoni
3
1
Kuhuisha vyupa vya maji safi vilivyotumika
Eneo la viwanda
4
127
Mashine za kusaga nafaka na cherehani
Mjini na Vijijini
Jumla
134

3.4 Uwekezaji katika sekta kilimo cha mbogamboga

 

Licha ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara, Wilaya pia ina maeneo makubwa na mazuri yanayofaa kwa kilimo cha mazao ya mbogamboga. Maeneo haya yana mabwawa ya umwagiliaji ila kuna changamoto ya uchakavu wa miundombinu

Jedwali 1: Maeneo ya kilimo cha mbogamboga

Na

Eneo 

Ukubwa wa eneo

1.

Matekwe

120

2.

Mitumbati

50

3.

Ntila

30

4.

Bonde la Ruponda

20

 

Jumla

220

4.4 Uwekezaji katika sekta ya mifugo

Wilaya ina maeneo mengi na makubwa ya uwekezaji katika mifugo kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 1.

Jedwali 2: Vijiji vilivyopimwa nakutengwa eneo la malisho

Na

Kijiji

Idadi ya Hekta

1

Likwela

                                       2,352.17

2

Nakalonji

                                       2,660.00

3

Chimbendenga

                                     7,918.04

4

Kilimarondo

                                      4,360.05

5

Namapwia

                                   1,345.93

6

Mtua

                                      1,836.81

7

Matekwe

                                   14,318.89

8

Kiegei

                                    2,337.32

9

Mbondo

                                       2,144.87

10

Maziwa

                                       2,096.32

11

Ngunichile

                                         158.00

12

Nahimba

                                          412.00

13

Namatunu

                                       1,004.00

14

Majonanga

                                       375.74

15

Makitikiti

                                      370.00

16

Ndomondo

                                       430.00

 

Jumla

                               44,120.14 

 

 

Uwekezaji katika sekta ya Elimu

 

Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea ina utaratibu wa kuwa na mradi mkubwa wa kujenga shule kubwa ya sekondari itakayoanzia kidato cha kwanza hadi cha sita, utaratibu wa kupata eneo la ujenzi wa shule hiyo unaendelea mkuu wa idara ya ardhi na maliasili anaendelea na utaratibu huo.

5.5 Maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa 

 

Mbali na maeneo ya ufugaji, Wilaya ina maeneo mengi ya uwekezaji kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na.2.

 

Jedwali 3: Maeneo ya uwekezaji


AINA YA UWEKEZAJI
MAHALI ENEO LILIPO
UKUBWA WA ENEO

1

ENEO LA VIWANDA
Viwanda viko kwenye ramani ya mipango miji taratibu za upimaji zinaendelea
Bondeni Area
81,000m2

2

HOUSING ESTATE
Maeneo yamepimwa lakini hayajalipiwa fidia
Bondeni Road
18,158m2 na 43,835m2 zipo kwe mpango wa upimwaji

3

MARKET
Eneo limeshapimwa tayari bado fidia
Bondeni Road
22,704m2

4

SCHOOLS
Maeneo yapo yamepimwa tayari na pia yako mengine ambayo hayajapimwa
Bondeni Road
83,481m2

5

MAENEO YA MADINI
Maeneo yametengwa maeneo yenye madini aina ya Dhahabu, Nickel, Chuma, Dhahaabu na Shaba.
Kijiji cha Marambo
1,639.46m2

6

MISITU
Wilaya ina misitu yenye miti aina mbalimbali. Raslimali za misitu zinasimamiwa kwa mbinu shirikishi ya uhifadhi wa mazao ya misitu ambapo mpaka sasa kupitia programu ya PFM jumla ya misitu 9 imetambuliwa na kukabidhiwa kwa jamii za vijiji 11.
Ndani ya Vijiji 11 kwa misitu 9
4,709,000 ha

7

UFUGAJI WA NYUKI
Kutokana na kuwepo na misitu ya asili ambayo inasaidia kuwepo kwa nyuki, Wilaya ina fursa ya kufuga nyuki kwa ajili ya kupata mazao yake ambayo ni muhimu kwa lishe.


8

MAENEO YA UJENZI WA MAJUMBA
Yapo maeneo ambazo yamepimwa lakini hayajalipiwa fidia na maeneo menging yapo kwemye mpango wa upimaji
Bondeni Road
18,158m2 na 43,835m2 zipo kwenye mpango wa upimaji

9

UTALII
Wilaya ina fursa kubwa ya uwekezaji hasa wa wanyamapori. Fursa hii pamoja na umuhimu wake haijaendelezwa ipasavyo na ikiendelezwa ni sehemu nzuri ya kihistoria ya ukombozi wa bara la Afrika hususani kwa nchi ya Msumbiji.  
Milima ya Ilulu, njia kuu ya wanyamapori toka Msanjesi hadi hifadhi ya wanyamapori ya Selous pamoja na kambi ya Farm 17 (Frelimo Freedom Fighters Camp).
Njia kuu ya wanyamapori ya Selous-Msanjesi ambayo ni kiunganisho na Lukwaka, Lumesule hadi hifadhi ya Nisassa iliyopo nchini Msumbiji

10

MAENEO YA UJENZI WA SHULE 
Yapo maeneo yaliyopimwa na yasiyopimwa
Bondeni Road
83,481m2

ENEO AMBALO LIPO KWENYE UTAFITI
Yapo maeneo ambayo yapo kwenye utafiti madini ambayo yanapatikana ni Nickel, Iron, Gold na Copper.

1607.94m2

4.0 HITIMISHO

Nia ya Wilaya ni kuona kila mwananchi anapata fursa ya uwekezaji katika moja ya maeneo yaliyoainishwa. Ni matumaini kuwa, fursa ya nchi yetu kuingia katika uchumi wa kati tutaitendea haki wana Nachingwea. Mshikamano wetu utaleta chachu kubwa katika kuinua uchumi wa Wilaya yetu na nchi kwa ujumla.

Shukrani kwa wakuu wa idara na vitengo, Taasisi za serikali kwa ushirikiano mlioutoa wakati mawasiliano ya kupata takwimu zilizotumika kuandaa tarifa hii.

IMEANDALIWA NA AFISA BIASHARA NACHINGWEA

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • NACHINGWEA DC YAKABIDHI JUKUMU LA UZOAJI TAKA KWA KAMPUNI YA KASANDRA CLEANING SERVICE

    March 16, 2023
  • DEO MSINGI AFANYA KIKAO CHA TATHIMINI YA ELIMU YA MWEZI JANUARI NA FEBRUARI 2023

    March 14, 2023
  • MKOA WA LINDI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE KUPITIA MIKOPO YA HALMASHAURI

    March 08, 2023
  • WAZAZI WA WANAFUNZI AMBAO HAWATAFANYA MITIHANI YA MUHULA KUHOJIWA OFISI ZA KATA

    February 08, 2023
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AKIZUNDUA MRADI WA MAJI NAMIKANGO
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.