Mwakilishi wa katibu Mkuu ofisi ya Rais TAMISEMI na Afisa kutoka ofis ya Rais TAMISEMI idara ya usimamizi wa elimu ndugu Upendo Rweyemamu amefanya kikao kazi na waalimu wa elimu msingi na sekondari pamoja na waratibu elimu kata, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa TTC Nachingwea June 1, 2024.
Bi Rweyemamu amewakumbusha walimu kutambua kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa wa sekta ya elimu wa kulea watoto, kuwapa ujuzi na kuwajenga maadili, kwa kutambua hilo serikali inashughulikia changamoto za walimu, sambamba na hilo serikali imepandisha madaraja ya mseleleko kwa walimu zaidi ya elfu hamsini na Madaraja ya lazima zaidi ya elfu elfu na tarehe 01/07/2024 yanaanza.
Amewataka walimu wote ambao walipandishwa madaraja na hawakulipwa stahiki zao wapeleke taarifa zao Jumatatu na kutilia mkazo mahusiano ili mwalimu aweze kutoa matokeo mazuri lazima kuwe na mahusiano mazuri baina yao na viongozi wao kinyume chake wanaenda kumaliza hasira kwa mwanafunzi na kuleta matokeo mabaya.
Aidha, bi Rweyemau amewataka walimu kuwaandaa wanaunzi kwa kuzingatia KKK katima madarasa ya misingi yaani darasa la kwanza la pili kwani Kunachangamoto watoto wanakwenda darasa la tatu hawajui kusoma wala kuandika wakati serikali inapambana ili kutoa elimu iliyo bora hivyo walimu ni lazma wajitoe.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.