Hayo yameelezwa Leo June 18, 2024 na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dunstan Kitandula katika ziara yake ya kikazi Wilaya ya Nachingwea ambapo ameeleza kuwa, Serikali inatambua changamoto ya wanyama wa tembo katika maeneo mengi ya Tanzania na sio Nachingwea pekee huku akihaidi upatikanaji wa mabomu hayo 700 ambayo yatasaidia kurudisha wanyama hao hifadhini.
Sambamba na mabomu 700 pia ameahidi upatikanaji wa gari moja kwa kila wilaya iliyokumbwa na hadha hiyo na kueleza kuwa chanzo cha tatizo hilo ni kuruhusu wafugaji kuvamia katika maeneo ya wanayama na tayari msako wa kuwaondoa wafugaji hao ushaanza kufanyika na kuwarejesha kwenye maeneo yao na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwenye hilo.
Aidha, Mheshimiwa Amandusi Chinguile ambae ni Mbunge wa jimbo la Nachingwea ameeleza kuwa Serikali inachukua hatua kuhakikisha wananchi wapo salama dhidi ya wanyama hao pamoja na upatikanaji wa vituo vya askari wanayamapori na Maafisa wake.
Nae Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mheshimiwa Mohamed Hassan Moyo amewahasa wananchi kuwa watulivu sambamba na kuwataka kujitokeza kwenye matibabu ya macho yatakayofanyika Julai 29 mpa 31 na madaktari bingwa wa macho katika Hospitali ya Wilaya ya Nachingwea.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.