• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

MHESHIMIWA MPYAGILA AMPONGEZA MHE. RAIS KWA KULETA FEDHA NYINGI SEKTA YA ELIMU WILAYANI NACHINGWEA

Imetumwa : March 20th, 2025

Tarehe 20 Machi, Mh. Adnan Mpyagila, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nachingwea, amefanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi wa shule za sekondari. Ameangalia ujenzi wa Shule ya Sekondari Kata  Mtua ,Kata Chiumbati, Rugwa Boys (mabweni), Shule ya Kata ya Nachingwea, na Shule ya Naipanga Sekondari, ambapo amefuatilia maendeleo ya uandikishaji wa wanafunzi wa kidato cha kwanza.

Mh. Mpyagila ametoa shukrani kwa Mhe. Rais kwa kuleta fedha nyingi katika sekta ya elimu katika wilaya ya Nachingwea. Amewataka wazabuni kuhakikisha wanakamilisha miradi kwa wakati ili watoto waweze kuripoti shule mpya na vifaa vipelekwe kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Aidha, Mh. Mpyagila amewahimiza wazazi ambao bado hawajawaleta watoto wao kujiunga na shule za sekondari, hususan wanafunzi wa kidato cha kwanza, kuhakikisha wanaripoti kwa wakati ili waweze kupata fursa ya masomo na kufaidika na uboreshaji unaofanywa katika sekta ya elimu wilayani. Alisisitiza kuwa elimu ni msingi wa maendeleo, na ni muhimu kwa watoto kujiunga na shule kwa manufaa ya familia na jamii kwa ujumla.


Kwa upande mwingine, Mwalimu Jonas Joas, Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Nachingwea, amesema imepokea shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya shule tatu za Sekondari zinazoendelea kujengwa , Shule ambazo zitasaidia kupunguza umbali mrefu wanaotembea wanafunzi. Alieleza kuwa changamoto za ucheleweshaji wa miradi zimetokana na wazabuni kujiondoa kwa sababu ya mtaji mdogo na usimamizi duni. Hata hivyo, alisema kuwa uandikishaji wa wanafunzi umefikia asilimia 94, huku wakiendelea kukabiliana na changamoto za uandikishaji katika maeneo yenye umbali mrefu.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • VIKUNDI 55 VYA WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% WAJENGEWA UWEZO

    July 03, 2025
  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% WATAKIWA KUWA NA NIDHAMU YA FEDHA, MILIONI 649 ZAKOPESHWA AWAMU YA PILI

    July 03, 2025
  • NACHINGWEA YAJIFUNZA MBINU BORA ZA USIMAMIZI WA MIGODI KUTOKA GEITA

    June 27, 2025
  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA USHIRIKI WA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA.

    June 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.