• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

NDITI NI KIJIJI KIKUBWA KINAHITAJI MIUNDOMBINU IMARA

Imetumwa : September 15th, 2025

Serikali ya kijiji cha Nditi, ikiongozwa na Mwenyekiti Salumu Amuli Husseni, ilifika katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea. Lengo la ziara hiyo lilikuwa kuwasilisha kero zinazowakabili wananchi, zikiwemo changamoto katika sekta ya afya, nishati na wanyamapori.

Wakiwa hapo, walikutana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, ambaye pia ni Afisa Mipango, Joshua Mnyang’ali. Mwenyekiti alieleza kuwa wodi ya wazazi katika zahanati ya kijiji haijakamilika, kijiji kinakosa huduma ya umeme, na tembo wamekuwa wakiingia kwenye makazi ya watu na mashamba yao.

Joshua Mnyang’ali aliwapongeza viongozi hao kwa kufuatilia maendeleo ya wananchi wao. Alieleza kuwa suala la wodi ya wazazi tayari lipo kwenye mpango wa utekelezaji na zabuni inatarajiwa kuanza mwezi wa tisa. Kwa upande wa umeme, TANESCO wanatarajiwa kufika kijijini wiki ijayo, na kuhusu tembo, halmashauri imenunua drone kwa ajili ya kuwafukuza.

Aidha, Joshua alieleza kuwa kijiji cha Nditi ni kikubwa na chenye fursa nyingi, hivyo kinahitaji miundombinu madhubuti. Alisema halmashauri itaangalia uwezekano wa kuingiza ujenzi wa Kituo cha Afya katika mpango wa maendeleo wa mwaka wa fedha 2026/2027.

Mwisho wa kikao, Mwenyekiti Salumu alitoa shukrani za dhati kwa ofisi ya Mkurugenzi kwa namna walivyopokea hoja zao. Aliomba pia kijiji hicho kitambuliwe rasmi uongozi wake, kutokana na juhudi wanazoendelea kufanya katika kusukuma gurudumu la maendeleo.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • NDITI NI KIJIJI KIKUBWA KINAHITAJI MIUNDOMBINU IMARA

    September 15, 2025
  • DED CHIONDA : WANANCHI TUMIENI TAMASHA LA ONE STOP CENTER KAMA FURSA

    September 11, 2025
  • CHIFU NAKOTYO KUONGOZA MAOMBI MAALUMU YA KULIOMBEA TAIFA KUELEKEA UCHAGUZI

    September 09, 2025
  • WAZEE NACHINGWEA WASISITIZA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

    September 09, 2025
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.