Mwenge wa Uhuru 2025 ukiongozwa na Mkimbiza Mwenge kitaifa ndugu Ismail Ali Ussi umemulika na kuleta matumaini Nachingwe Mei 29, 2025.
Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la Msingi katika Mradi wa ujenzi wa Shule ya sekondari ya Kata ya Chiumbati shuleni iliyopo katika Kijiji cha Luagala wenye thamani ya Milioni 560, Shule hii imeleta tumaini jipya na kutatua kazia ya muda mrefu ya kutokua na Shule katika kata hiyo kwani hapo awali wanafunzi walilazimika kutembe umbali usiopongua Kilomita 5 hadi 7 kufuata shule ya Sekondari.
Kwa upande mwingine kwa kuzingatia usalama wa raia na mali zao jeshi la Polisi lilianzisha mradi wa kituo kidogo cha Polisi cha kata hiyo chenye thamni ya Shilingi milio 81.1 ambacho kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa ameonesha kufurahishwa na ubora wa mradi huo na kukubali kuweka jiwe la Msingi, kituo hicho kipo katika hatua za mwisho kabisa ili kianze kutumika kwani kimekamilika kwa zaidi ya 90%.
Katika kuendelea kuwaletea maendeleo wananchi Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Daktari Samia Suluhu Hassan imetatua kero kubwa ya maji iliyodumu kwa zaidi ya miaka kumi (10) katika Kata ya Raha leo, Naipanga na Chiumbati shuleni kwa kujenga mradi wenye thamani ya Shilingi 1,187,000,000 unaofahamika kama Mradi wa Maji Naipanga wenye ujazo wa lita 300,000 ambao Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa ndugu Ussi ameuzindua, mradi huu unahudumia zaidi ya wakazi 12,999 katika vijiji vya Naipanga,Chiumbati Shuleni, Chiwindi, Tandika, Luagala, Rahaleo, Maendeleo, Kilombero, Nagaga, Joshoni, na Chekeleni
Mwenge wa Uhuru umekata kiu ya muda mrefu ya wakazi wa kijiji cha Naipingo kwa kuweka jiwe la Msingi katika Zahanati mpya ya kijiji hicho yenye thamani ya Shilingi milioni 50 za mapato ya ndani, wananchi wa Naipingo wamekua na hamu kubwa ya kupata huduma za afya katika eneo lao kwani wamekua wakilazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.
Pia,umeweka Jiwe la Msingi katika ujenzi wa barabara ya KKT-Hospitali ya kiwango cha lami yenye urefu wa km 0.5 na thamani ya Shilingi milion 356, pia umetembelea na kuona shughuliza utengenezaji wa samani unaofanywa na kikundi cha vijana kinachofahamika kama UWASO ambacho kilikopa Sh Mil 50.
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.