• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko/mrejesho |
Nachingwea District Council
Nachingwea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii Vijana na Ustawi wa Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Ugani
  • Madiwanii
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Ujenzi uchumi na mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI WA WILAYA YA NACHINGWEA AWAPA SEMINA WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA (36) NA NGAZI YA KIJIJI (127)

Imetumwa : September 30th, 2024

Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata na Vijiji wilayani Nachingwea wamepata mafunzo ya uchanguzi wa serikali za mitaa yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo wa kusimamia na  kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 27 Novemba 2024, mafunzo hayo yaliyoendeshwa na Msimamizi wa Uchaguzi yamefanyika  leo tarehe 30 Septemba 2024.

Msimaizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mhandisi Chionda A. Kawawa amewataka wasimamizi hao wasaidizi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuhamasisha wananchi kujiandikisha ili wawe kwenye orodha ya wapiga kura, pia  amewasisitizia  kuwa wanajukumu la kuwakumbusha wananchi kuhusu umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.

Katika semina hii muhimu, Msimamizi wa Uchaguzi amewakaribisha washiriki wote kushiriki kwa sababu uchaguzi huu ni fursa ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii na amewasisitiza kutekeleza majukumu hayo kwa kujiamini kwa ufanisi, akisema, "Tumeaminiwa kuwa tuna uwezo wa kufanya kazi hii."


Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Nachingwea ndugu Robert Mmali amewataka washiriki kutoa elimu sahihi na kufuata kanuni na miongozo iliyowekwa. "Someni muelewe, na msijifanye kuwa na uelewa bila msingi. Ulizeni ili kupata majibu sahihi," .


Wasimamizi wa ngazi za Kata na Vijiji wanatarajiwa kujadili umuhimu wa uchaguzi, kuhamasisha wananchi kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali, na umuhimu wa kupiga kura kumchagua kiongozi mwenye sifa kwa ajili ya maendeleo ya jamii, amesisitiza kuwa uchaguzi huu unapaswa kufanyika katika mazingira huru, wazi, na salama.


Aidha, Mhandisi Chionda amesema watakaoonesha ufanisi katika uandikishaji na kuvuka malengo watapewa zawadi kama motisha ya kuongeza ari na ubunifu katika kazi zao.


Katika semina ya uchaguzi wa serikali za mitaa, washiriki walionesha dhamira yao ya kuendelea kuhamasisha wananchi kujiandikisha na kushiriki uchaguzi. Walisema kuwa kila mwananchi aliyefikia umri wa miaka 18 anapaswa kushiriki katika mchakato huu wa kidemokrasia.


Wakisisitiza umuhimu wa uchaguzi wa huru na haki, washiriki walikubaliana kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAOITWA KWENYE MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI March 26, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 16 NA DERAVA DARAJA II NAFASI NNE May 25, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WALIOOMBA AJIRA ZA UTENDAJI WA KIJIJI NA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA July 22, 2022
  • Tangazo la kazi za muda December 27, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANAFUNZI WA NACHINGWEA HIGH NA RUGWA BOYS WAAGWA KWA HAFLA FUPI, WAJIANDAA KWA MITIHANI YA TAIFA

    April 26, 2025
  • SDA NA LIIKE WATOA MAFUNZO YA HUDUMA YA KWANZA KWA MANGALIBA NA WALOMBO KWA AJILI YA KUIMARISHA UTAMADUNI SALAMA

    April 28, 2025
  • DED NACHINGWEA : AAGIZA MIRADI KUKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA KUZINGATIA VIWANGO

    April 09, 2025
  • RC LINDI : MIRADI YOTE ITAKAYOPITIWA NA MWENGE IZINGATIE MATUMIZI BORA YA FEDHA

    April 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Wakulima wasisitizwa kulima mazao ya chakula
Video za mpya

Kurasa za Haraka

  • Opras Form
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea Eng. Chionda Alli Mfaume akizungumza waluu wa idara
  • MRADI WA MAJI NAMIKANGO WAZINDULIWA
  • Mpango wa Bajeti
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2021
  • UANZISHWAJI WA BLOCK FARMING WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA
  • MRADI WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 1 WAANZA KUTEKELEZWA NAIPANGA
  • Sheria za Fedha za Mitaa
  • Sheria za Halmashauri

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TUZO ZA ELIMU WILAYA YA NACHINGWEA
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.