Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Mohamed Hassan Moyo, amewataka maafisa ugani kusimamia ipasavyo majukumu yao ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao kwa kutumia pembejeo na viuatilifu vinavyotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Maelekezo hayo yametolewa leo Juni 9, 2025 katika kikao kazi kilichowakutanisha maafisa ugani, watendaji wa kata na meneja wa AMCOS, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea.
Mkuu wa Wilaya amesema matarajio ni kuona ongezeko la uzalishaji kutokana na upatikanaji wa pembejeo kwa wakati na kwa kiwango cha kutosha.
Aidha, amewapongeza watendaji wa kata na mameneja wa AMCOS kwa ushiriki wao mzuri katika Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025, akisema hatua hiyo ni ishara ya mshikamano na uwajibikaji.
#Tupovizuri
Copyright ©2018 Nachingwea District Council. All rights reserved.